• HABARI MPYA

    Friday, December 08, 2023

    TANZANIA BARA YATWAA NAFASI YA TATU CECAFA U18, UGANDA BINGWA


    TANZANIA Bara imemaliza nafasi ya tatu katika michuano ya vijana chini ya umri wa miaka 18 (CECAFA U18) leo baada ya ushindi wa 3-1 dhidi ya Rwanda Uwanja wa Jomo Kenyatta mjini Kisumu nchini Kenya.
    Mabao ya Tanzania Bara inayofundishwa na kocha yamefungwa na Zidane Ally dakika ya 19, Said Said dakika ya 26 na Misheto dakika ya 49, wakati la Rwanda limefungwa na Didier dakika ya 37.
    Katika mchezo wa Fainali Uganda wamefanikiwa kubeba taji hilo kwa ushindi wa 2-1 dhidi ya wenyeji, Kenya katika mchezo uliokwenda hadi dakika ya 120 kufuatia sare ya 1-1 ndania ya dakika 90 hapo hapo Uwanja wa Jomo Kenyatta.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TANZANIA BARA YATWAA NAFASI YA TATU CECAFA U18, UGANDA BINGWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top