• HABARI MPYA

    Saturday, December 16, 2023

    GEITA GOLD NA NAMUNGO ZASONGA MBELE KIBABE AZAM FEDERATION CUP


    TIMU ya Geita Gold imefanikiwa kutinga Hatua ya 32 Bora Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) baada ya ushindi wa mabao 5-0 dhidi ya Singida Cluster katika mchezo uliofanyika leo Uwanja wa shule ya sekondari ya wasichana ya Nyankumbu mjini Geita.
    Mabao ya Geita Gold yamefungwa na Tariq Seif dakika ya 14 na 19, Mwaita Gereza dakika ya 47, George Sangija dakika ya 49 na Geofrey  Julius dakika ya 90 na ushei.
    Mechi nyingine za ASFC leo, Namungo imeitupa nje Hollywood kwa kuichapa mabao 5-0 Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi.
    Mabao ya Namungo FC yamefungwa na James Mwashinga dakika ya 23, Kelvin Sabato dakika ya nane kwa penalti, 36 na 63 na Michael Joseph dakika ya 77.
    Nayo Tabora United imeichapa Coffee ya Mwadui 4-1 Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora huku jirani zao, Mashujaa FC wakiilaza Mbuga FC 3-2 Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma.
    MATOKEO YOTE MECHI 64 BORA ASFC
    DESEMBA  16, 2023
    Namungo FC 5-0 Hollywood FC
    Geita Gold 5-0 Singida Cluster
    Mashujaa FC 3-2 Mbuga FC
    Tabora United 4-1 Coffee Monduli
    Pan Africans 1-2 Nyamongo SC
    Biashara United 4-1 THB FC
    FGA Talents 2-0 Buhaya FC
    Polisi Tanzania 2-1 Nyumbu FC 
    Pamba FC 1-0 Eagles SC
    Green Warriors 4-1 Kilimo FC
    Mbuni FC 6-2 Bus Stand
    Tanzania Prisons 0-0 TRA Kilimanjaro (Penalti 5-6)
    DESEMBA  15, 2023
    Singida Fountain 3-0 Arusha City 
    Ken Gold 0-1 Gunners FC 
    Transit Camp 2-0 Airport FC 
    Cosmopolitan 1-2 Rhino Rangers imewatoa
    DESEMBA  14, 2023
    Dodoma Jiji FC 1-0 Magereza Dar
    JKT Tanzania 5-0 Kurugenzi Simiyu 
    Ihefu SC 3-0 Rospa FC  
    Coastal Unión 2-0  Greenland  
    MECHI ZA LEO DESEMBA 17, 2023
    Mbeya City v African Lyon Sokoine, Mbeya
    Cocpo FC v Mabao FC Nyamagana, Mwanza
    Ruvu Shooting v Mkwajuni FC Jamhuri, Morogoro
    TMA FC v Sharp Lion, Sheikh Amri Abeid, Arusha
    KMC FC v ACA Eagle Uhuru, Dar es Salaam
    Azam FC v Allianve FC, Azam Complex, Chamazi
    MECHI ZA MWISHO ZITATAPANGIWA TAREHE
    Yanga SC v Housing FC (Njombe)    
    Simba SC v Tembo FC (Tabora)
    Mtibwa Sugar v Nyakagwe (Geita)
    Kagera Sugar v Dar City
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: GEITA GOLD NA NAMUNGO ZASONGA MBELE KIBABE AZAM FEDERATION CUP Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top