• HABARI MPYA

    Sunday, July 19, 2026

    NI ENGLAND WASHINDI WA TATU KOMBE LA DUNIA 2026


    TIMU ya England imefanikiwa kumaliza nafasi ya Tatu Kombe la Dunia baada ya ushindi wa mabao 6-4 dhidi ya Ufaransa usiku wa kuamkia leo Uwanja wa Hard Rock Jijini Miami Gardens, Florida nchini Marekani.
    Mabao ya Three Lions yamefungwa na kiungo wa Arsenal, Declan Rice dakika ya tatu, beki wa Aston Villa, Ezri Ngoyo Konsa mwenye asili ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) dakika ya 18, winga wa Arsenal, Bukayo Ayoyinka Temidayo Moses Saka mwenye asili ya Nigeria, matatu dakika ya 37, 45+1  na  la penalti dakika ya 87 huku lingine likifungwa na kiungo wa Real Madrid, Jude Victor William Bellingham mwenye asili ya Kenya dakika ya 90’+8.
    Kwa upande wa Ufaransa mabao yao yamefungwa na washambuliaji, Kylian Mbappé Lottin wa Real Madrid mwenye asili ya Cameroon, mawili dakika ya  48 na  66, Bradley Jean-Manuel Essolisam Addo Barcola wa mwenye asili ya Togo dakika ya 54 na Masour Ousmane Dembélé mwenye asili ya Senegal - Mauritania na na Mali dakika ya 90’+6 wote wa Paris Saint-Germain.
    Kwa kufunga mara mbili kwenye mchezo huo, Mbappé amefikisha mabao 10, mawili zaidi ya Lionel Messi wa Argentina ambaye baadaye Saa 4:00 usiku wa leo ataiongoza timu yake katika mchezo wa Fainali dhidi ya Hispania Uwanja wa MetLife, East Rutherford, Bergen County, New Jersey hapo hapo Marekani.
    Next
    This is the most recent post.
    Older Post
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NI ENGLAND WASHINDI WA TATU KOMBE LA DUNIA 2026 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top