• HABARI MPYA

    Saturday, December 30, 2023

    AZAM FC YAWACHAPA CHIPUKIZI 1-0 NA KUONGOZA KUNDI A MAPINDUZI


    BAO pekee la mshambuliaji Msenegal, Alassane Diao dakika ya 12 limeipa Azam FC ushindi wa 1-0 dhidi ya Chipukizi United katika mchezo wa Kundi A Kombe la Mapinduzi usiku huu Uwanja wa New Amaan Complex, Zanzíbar.
    Ushindi huo unaifanya Azam FC iongoze kundi hilo kwa pointi zake nne sasa ikifuatiwa na mabingwa watetezi, Mlandege na Vital’O ya Burundi zenye pointi mbili kila moja, wakati Chipukizi United sasa inashika mkia kwa pointi yake moja.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC YAWACHAPA CHIPUKIZI 1-0 NA KUONGOZA KUNDI A MAPINDUZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top