// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); ARSENAL YAUA 4-1 ULAYA NA KUTINGA 16 BORA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE ARSENAL YAUA 4-1 ULAYA NA KUTINGA 16 BORA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Wednesday, December 10, 2014

    ARSENAL YAUA 4-1 ULAYA NA KUTINGA 16 BORA

    KLABU ya Arsenal imefanikiwa kumaliza katika nafasi ya pili kwenye Kundi D, Ligi ya Mabingwa Ulaya na kutinga hatua ya 16 Bora ya michuano hiyo kufuatia ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya wenyeji Galatasaray nchini Uturuki.
    Lukas Podolski aliifungia The Gunners bao la kwanza dakika ya tatu, kabla ya Aaron Ramsey kufunga la pili dakika ya 11 na la tatu dakika ya 29.
    Kiungo mkongwe wa Uholanzi, Wesley Sneijder aliifungia Galatasaray bao la kufutia machozi kwa shuti la mpira wa adhabu dakika ya 87, kabla ya Padolski kufunga la nne kwa Arsenal dakika ya 90. 
    Mechi nyingine ya kundi hilo, Borussia Dortmund imetoka sare ya 1-1 na Anderlecht ya Ubelgiji.
    Kikosi cha Arsenal kilikuwa: Szczesny, Debuchy/O'Connor dk77, Mertesacker, Chambers, Bellerin, Flamini/Zelalem dk45, Oxlade-Chamberlain, Ramsey/Maitland-Niles dk45, Campbell, Podolski na Sanogo.
    Galatasaray: Sinan, Camdal/Alintop dk45, Kaya, Balta, Telles, Melo, Colak, Bruma/Adin dk77, Yilmaz/Oztekin dk45, Sneijder, Bulut na Hamzaoglu.
    Lukas Podolski (9) pretends to polish Ramsey's boot as the Arsenal stars hail the Welshman for his strike
    Lukas Podolski (jezi namba 9) akiigiza kupangusa kiatu Ramsey baada ya kuifungia Arsenal 
    Lukas Podolski fires past Galatasaray defender Semih Kaya to give Arsenal an early lead in the Group D clash
    Lukas Podolski akifumua shuti mbele ya beki wa Galatasaray, Semih Kaya kuifungia Arsenal 

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-2867516/Galatasaray-1-4-Arsenal-Lukas-Podolski-strike-sparks-Gunners-stroll-Aaron-Ramsey-scores-stunning-volley-Wesley-Sneijder-bags-consolation-free-kick.html#ixzz3LRXEefIv 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSENAL YAUA 4-1 ULAYA NA KUTINGA 16 BORA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top