// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); MBUYU TWITE ANAANZA MAZOEZI LEO - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE MBUYU TWITE ANAANZA MAZOEZI LEO - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Monday, December 22, 2014

    MBUYU TWITE ANAANZA MAZOEZI LEO

    Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM
    KIUNGO wa kimataifa wa Rwanda, Mbuyu Twite anatarajiwa kuanza mazoezi leo, baada ya kuwa nje kwa wiki moja kufuatia kuumia kifundo cha mguu.
    Mbuyu Twite anayeweza kucheza kama beki wa pembeni na kati pia, aliumia Desemba 13 akiichezea klabu yake, Yanga SC dhidi ya mahasimu, Simba SC katika mechi ya Nani Mtani Jembe.
    Mbuyu Twite aligongwa na beki wa Simba SC, Nassor Masoud ‘Chollo’ na kushindwa kuendelea na mchezo, nafasi yake ikichukuliwa na Hassan Dilunga dakika ya 39, wakati huo tayari Yanga SC imefungwa 1-0 na mwisho wa mchezo ikalala 2-0. 
    Mbuyu Twite kushoto anaanza mazoezi leo

    Baada ya mapumziko na tiba ya wiki nzima, mchezaji huyo wa zamani wa APR ya Rwanda yuko tayari kurudi kazini, klabu yake ikikabiliwa na mchezo mgumu dhidi ya mabingwa watetezi, Azam FC Desemba 28, mwaka huu.
    Kurudi mapema kwa Twite ni faraja kwa Yanga SC, kwani tayari itamkosa Nahodha wake, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ anayetumikia adhabu ya kadi nyekundu. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MBUYU TWITE ANAANZA MAZOEZI LEO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top