• HABARI MPYA

    Sunday, December 28, 2014

    JOHN TERRY APEWA MKATABA MPYA CHELSEA

    BEKI John Terry atasaini Mkataba wa mwaka mmoja kuendelea kuitumikia Chelsea baada ya kocha Mreno, Jose Mourinho kusema mpango huo unaandaliwa.
    Beki huyo wa kati mwenye umri wa miaka 34 ataongoza mbio za kuwania tuzo ya Mchezaji Bora wa Mwa wa Kulipwa (PFA) kutokana na kufanya kwake vizuri hivi sasa akicheza katika safu ya ulinzi. 
    Chelsea have acted quickly to reassure John Terry that he will remain at Stamford Bridge
    Chelsea imemuhakikishia mkongwe John Terry kuendelea na kazi Stamford Bridge

    Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho amesema jana kwamba Terry bado mchezaji muhimu kwake. "Hakuna shaka atapewa Mkataba mwingine. Nafahamu hilo, anafahamu pia. Tupo katika klabu, katika bodi tunafahamu hilo na pia unatakiwa kufikiria hilo,".
    "Bila sisi kuthibitisha hilo, unatakiwa ufikirie hivyo. Ni mchezaji muhimu sana katika timu, hivyo mkataba mpya unakuja haraka iwezekanavyo. Ni utaratibu tu," amesema.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: JOHN TERRY APEWA MKATABA MPYA CHELSEA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top