VIONGOZI na wachezaji wa Yanga SC baada ya sala ya Eid El Fitri leo Jijini Dodoma ambako wapo kwa ajili ya mchezo wa mwisho wa Hatua ya 16 Bora ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) dhidi ya wenyeji, Dodoma Jiji FC leo kuanzia Saa 2:00 usiku Uwanja wa Jamhuri.
Tayari timu saba zimetinga Robo Fainali ya michuano hiyo ambayo sasa inajulikana kama CRDB Bank Federation Cup ambazo ni Mashujaa FC, Azam FC, Singida Black Stars, zamani Ihefu SC, Coastal Union, Namungo FC, Geita Gold na Tabora United.
GONGA KUTAZAMA PICHA ZAIDI
0 comments:
Post a Comment