• HABARI MPYA

    Wednesday, April 24, 2024

    YANGA NA TABORA MEI MOSI CRDB BANK FEDERATION CUP



    MABINGWA watetezi, Yanga SC watamenyana na Tabora United Mei 1 katika Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), michuano ambayo sasa inajulikana kama CRDB Bank Federation Cup Uwanja wa Azam Complex, Dar es Salaam kuanzia Saa 2:30 usiku.
    Mchezo huo utatanguliwa na michezo miwili siku hiyo ya Robo Fainali ya CRDB Bank Federation Cup kati ya Ihefu SC na Mashujaa Saa 10:00 jioni Uwanja wa LITI mjini Singida na Coastal Unión dhidi ya Geita Gold Saa 12:15 jioni Uwanja wa  Mkwakwani Jijini Tanga.
    Hatua ya Robó Fainali ya CRDB Bank Federation Cup  itakamilishwa Mei 3 kwa mchezo kati ya Azam FC na Namungo FC Saa 1:00 usiku Uwanja Azam Complex.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA NA TABORA MEI MOSI CRDB BANK FEDERATION CUP Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top