BEKI Lusajo Elukaga Mwaikenda ameongeza mkataba wa miaka miwili kuendelea na kazi Azam FC ambao utamuweka viunga vya Azam Complex hadi mwaka 2027.
Mwaikenda (23) ni zao lingine la uwekezaji katika soka ya vijana Azam FC ambaye baada ya kufanya vizuri Azam Academy alipelekwa KMC kwa mkopo Agosti 2020 kupata uzoefu kabla ya kurejea Juni mwaka Juni 2021 na moja kwa moja kuingia kikosi cha kwanza na kuaminiwa kiasi cha kuteuliwa Nahodha Msaidizi.
GONGA KUTAZAMA PICHA ZAIDI
0 comments:
Post a Comment