• HABARI MPYA

    Tuesday, April 09, 2024

    SIMBA SC YATOLEWA KWA MATUTA KOMBE LA TFF


    VIGOGO, Simba SC wametupwa nje ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) baada ya kufungwa na wenyeji, Mashujaa FC kwa penalti 6-5 kufuatia sare ya kufungana bao 1-1 ndani ya dakika 90 jioni ya leo Uwanja wa Lake Tanganyika mjini Kigoma.
    Mashujaa walitangulia kupata bao kupitia kwa mshambuliaji wake Reliant Rusajo dakika ya tano akimalizia pasi ya 60 Omar Omar, kabla ya mshambuliaji Muivory Coast , Freddy Koubalan kuisawazishia Simba dakika ya 51 akimalizia kazi nzuri ya Kibu Dennis.
    Mashujaa ilimaliza pungufu baada ya kiungo wake Said Juma ‘Makapu’ kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 45+2.
    Kipa wa zamani wa Yanga, Eric Johola ndiye aliyeibuka shujaa kwa kupangua penalti mbili za Simba zilizopigwa na viungo, Mcameroon Leandre Willy Essomba Onana na Mmali, Sadio Kanoute.
    Waliofunga penalti za Mashujaa ni Sansón Madeleke, Michael Masinda, Idrisa Stambuli, Adam Adam, Mpoki Mwakinyuke na Baraka Mtui, huku Zuberi Dabi pekee akikosa.
    Kwa upande wa Simba waliofunga ni Nahodha Mohamed Hussein 'Tshabalala', Israel Mwenda, Freddy Koublan, Muzamil Yassin na Ladack Chasambi.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA SC YATOLEWA KWA MATUTA KOMBE LA TFF Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top