// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); BALOTELLI ALIZUA TENA ENGLAND, SAFARI HII KWENYE INSTA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE BALOTELLI ALIZUA TENA ENGLAND, SAFARI HII KWENYE INSTA - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Tuesday, December 02, 2014

    BALOTELLI ALIZUA TENA ENGLAND, SAFARI HII KWENYE INSTA

    MSHAMBULIAJI wa Liverpool, Mario balotelli anakabiliwa na hatari ya kufungiwa mechi na FA baada ya kuposti ujumbe wa kibaguzi kwenye akaunti yake ya Instagram.
    Mshambuliaji huyo wa Italia aliposti picha katika akaunti yake ya Instagram ya mchezo wa game wa Super Mario inayosomeka: 'Usiwe mbaguzi — kuwa kama Mario. Ni fundi wa Kitaliano aliyetengenezwa na watu wa Japan wanaozungumza Kiingereza na kuonekana kama wa Wamexico,”.
    Na chini ya picha hiyo kulikuwa kuna maneno yasemayo: '... Ruka kama mtu mweusi na kamata sarafu kama Mnahudi,”.'
    Balotelli mwenye umri wa miaka 24, akijibu shutuma dhidi yake kutokana na ujumbe wake mtandaoni aliandika tena ujumbe usemao; “Mama yangu ni Myahudi, wote nyamazeni kimya”.
    Hata hivyo, Balotelli anadaiwa kuufuta haraka haraka ujumbe wa awali aliouandika ambao unadaiwa kuwa ni wakibaguzi. Msemaji wa Liverpool, amekiri kuwa na taarifa ya ujumbe huo na kwamba watafanya mazungumzo na Balotelli.
    FA ya England imesema ina taarifa za mchezaji huyo kuiweka taarifa hiyo katika Instagram kabla ya kuifuta baadaye kidogo.

    Balotelli could face a five-match ban if he is charged by the FA
    Nyota wa Liverpool, Mario Balotelli ameposti picha jana ambayo inaweza kumsababishia matatizo
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BALOTELLI ALIZUA TENA ENGLAND, SAFARI HII KWENYE INSTA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top