BAO pekee la Paul Peter dakika ya 71 limeipa Dodoma Jiji FC ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, JKT Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi Jijini Dar es Salaam.
Kwa ushindi huo, Dodoma Jiji FC wanafikisha pointi 12 na kupanda nafasi ya nne, wakati JKT inayobaki na pointi zake 11 pia inashukia nafasi ya sita ikizidiwa baada ya wote kucheza mechi nane.
0 comments:
Post a Comment