• HABARI MPYA

    Thursday, October 19, 2023

    AISHI ANAVYOANDALIWA KUZUIA MICHOMO YA AL AHLY KESHO DAR


    KIPA namba moja wa Simba SC, Aishi Manula akidaka mpira mbele ya wasaidizi wake wakati wa mazoezi ya jana Uwanja wa Mo Simba Afrena Jijini Dar es Salaam kuelekea mchezo wake wa kwanza wa Ligi ya Soka Afrika (AFL) dhidi ya Al Ahly ya Misri kesho Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
    Simba SC ina jumla ya makipa wanne, mbali na Aishi wengine ni Mmorocco Ayoub Lakreb, Ally Salum, Hussein Abel na Ally Ferouz.
    Timu hizo zitarudiana Jumanne ijayo, Oktoba 24 Uwanja wa Cairo International na mshindi wa jumla atakwenda Nusu Fainali ambako atakutana na mshindi wa jumla kati ya Petro de Luanda na Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini.
    PICHA: MAZOEZI YA SIMBA SC JANA JIJINI DAR ES SALAAM

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AISHI ANAVYOANDALIWA KUZUIA MICHOMO YA AL AHLY KESHO DAR Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top