WENYEJI, Polisi Tanzania wamelazimishwa sare ya 0-0 na Ruvu Shooting katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo Uwanja wa Ushirika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.
Kwa matokeo hayo katika mchezo wa 19 kwa kila timu, Polisi Tanzania inafikisha pointi 11, ingawa inaendelea kushika mkia ikizidiwa pointi mbili na Ruvu Shooting ya juu yake kwenye ligi ya timu 16.
Ikumbukwe timu mbili zitateremka Daraja mwisho wa msimu na mbili zinakwenda kwenye mchujo wa kuwania kubaki Ligi Kuu.
0 comments:
Post a Comment