• HABARI MPYA

    Tuesday, January 03, 2023

    BRENTFORD YAICHAPA LIVERPOOL 3-1 GTECH


    WENYEJI, Brentford City wameibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Liverpool katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa jana Uwanja wa Gtech Community.
    Mabao ya Brentford la kwanza alijifunga Ibrahima Konate dakika ya 19, la pili akafunga Yoane Wissa  dakika ya 42 na la tatu Bryan Mbeumo dakika ya 84, wakati la Liverpool limefungwa na Alex Oxlade-Chamberlain dakika ya 50.
    Kwa ushindi huo, Brentford inafikisha pointi 26 katika mchezo wa 18 na kusogea nafasi ya saba ikizidiwa pointi mbili na Liverpool ambayo hata hivyo ina mechi moja mkononi.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BRENTFORD YAICHAPA LIVERPOOL 3-1 GTECH Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top