• HABARI MPYA

    Friday, January 13, 2023

    FULHAM YAITANDIKA CHELSEA 2-1 LONDON


    WENYEJI, Fulham wameibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Chelsea katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jana Uwanja wa Craven Cottage Jijini London.
    Mabao ya Fulham yamefungwa na Willian dakika ya 25 na Carlos Vinicius dakika ya 73, wakati la Chelsea limefungwa na Kalidou Koulibaly dakika ya 47.
    Kwa matokeo hayo, Fulham inafikisha pointi 31 katika mchezo wa 19 ikisogea nafasi ya sita, wakati Chelsea inabaki na pointi zake 25 za mechi 18 nafasi ya 10.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: FULHAM YAITANDIKA CHELSEA 2-1 LONDON Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top