TIMU ya Namungo FC imepata ushindi wa ugenini wa mabao 3-1 dhidi ya wenyeji, KMC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.
Mabao yote ya KMC leo yamefungwa na mshambuliaji wake Ibrahim Mkoko dakika za 40, 57 na 90 na ushei.
Kwa ushindi huo, Namungo FC inafikisha pointi 29, ingawa inabaki nafasi ya sita, wakati KMC inabaki na pointi zake 23 nafasi ya 10 baada ya wote kucheza mechi 21.
0 comments:
Post a Comment