KLABU ya Al Hilal ya Sudan inatarajiwa kuwasili nchini kesho kuweka kambi ya kujiandaa na michezo ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Ikiwa nchini, Al Hilal itacheza mechi tatu za kirafiki ikiwemo dhidi ya wenyeji wao, Simba SC Februari 5, mwaka huu Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Kabla ya hapo, Hilal itacheza Namungo FC Januari 26 na Azam FC Januari 31 katika mechi nyingine mbili za kirafiki Uwanja wa Azam Complex Jijini Dar es Salaam.
0 comments:
Post a Comment