TIMU ya Manchester United imefanikiwa kwenda Raundi ya Nne ya Kombe la FA England baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Everton usiku wa Ijumaa Uwanja wa 3-1 Old Trafford Jijini Manchester.
Mabao ya Mashetani hao Wekundu yamefungwa na Antony dakika ya nne, Conor Coady aliyejifunga dakika ya 52 ambaye pia alifunga bao la Everton dakika ya 14 na Marcus Rashford kwa penalti dakika ya 90 na ushei.
0 comments:
Post a Comment