KLABU ya Yanga SC imemtambulisha beki wa kati, Mamadou Doumbia (27) kutoka Stade Malien ya kwao kuwa mchezaji wake mpya dirisha hili dogo.
Doumbia anayefanya nyota wawili kwenye kikosi cha Yanga kutoka timu ya taifa ya Mali baada ya kip Djigui Diarra, anakuwa mchezaji mpya wa tatu dirisha hili dogo akiungana na kiungo Mzanzibari Mudathir Yahya na mshambuliaji Mzambia, Kennedy Musonda.
Doumbia aliibukiia Stade Malien mwaka 2015 kabla ya kwenda Olympique Safi ya Morocco mwaka 2017 aliporejea Stade Malien.
0 comments:
Post a Comment