RAIS wa heshima wa Simba SC, Mohamed Dewji ‘Mo Dewji’ leo ametembelea kambi ya mazoezi ya klabu Rais wa mjini Dubai, Falme za Kiarabu (UAE) na kufanya mazungumzo na wachezaji na benchi la ufundi.
Kilikuwa ni kikao kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo kuweka mikakati ya kuhakikisha Simba inatwaa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Afrika.
Mo Dewji ndiye ameipeleka timu Dubai ili kupata nafasi nzuri ya kufanya mazoezi chini ya kocha mpya, Mbrazil Robert Oliveira ‘Robertinho’.
0 comments:
Post a Comment