TIMU ya Arsenal imefanikiwa kwenda Raundi ya Nne ya Kombe la FA England baada ya ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya wenyeji, Oxford United usiku wa Jumatatu Uwanja wa The Kassam mjini Oxford, Oxfordshire.
Mabao ya Arsenal yamefungwa na Mohammed Elneny dakika ya 63 na Eddie Nketiah mawili dakika ya 71 na 76 na sasa mabingwa hao mara 14 wa Kombe la FA watamenyana na Manchester City iliyoitoa Chelsea.
0 comments:
Post a Comment