WENYEJI, Coastal Union wameibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya Polisi Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.
Bao pekee la Coastal Union limefungwa na Abdul Suleiman ‘Sopu’ dakika ya 21 na kwa ushindi huo Wagosi wa Kaya wanafikisha pointi 24 katika mchezo wa 22 na kupanda nafasi ya 12 kutoka mkoani.
Polisi Tanzania inabaki na pointi zake 25 za mechi 21 nafasi ya 10.
0 comments:
Post a Comment