WENYEJI, Chelsea wamelazimishwa sare ya 2-2 na Wolverhampton Wanderers katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa Jumamosi Uwanja wa Stamford Bridge Jijini London.
Mabao ya Chelsea yamefungwa na
Romelu Lukaku kwa penalti dakika ya 56 na 58 akimalizia pasi ya Christian Pulisic, wakati ya Wolves yamefungwa na Trincão dakika ya 79 na Conor Coady dakika ya 90 na ushei.
Kwa sare hiyo, Chelsea inafikisha pointi 67 mechi ya 35, ingawa inabaki nafasi ya tatu, wakati Wolves imefikisha pointi 50 katika mechi ya 35 pia nafasi ya nane.
0 comments:
Post a Comment