• HABARI MPYA

    Thursday, May 12, 2022

    KMC YACHAPA MTIBWA SUGAR 3-2 UHURU


    WENYEJI, KMC wameibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara mchana wa leo Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.
    Mabao ya KMC yamefungwa na Matheo Anthony mawili dakika ya 21 na 81 na Hassan Kessy dakika ya 73, wakati ya Mtibwa Sugar yamefungwa na George Makang'a dakika ya 13 na Ismail Mhesa kwa penalti dakika ya 41.
    Kwa ushindi huo, KMC inafikisha pointi 27 na kusogea nafasi ya 10, wakati Mtibwa Sugar inabaki na pointi zake 27 nafasi ya tisa baada ya wote kucheza mechi 23, wakitofautiana tu wastani wa mabao.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: KMC YACHAPA MTIBWA SUGAR 3-2 UHURU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top