TIMU ya Azam FC imeibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya wenyeji, Mtibwa Sugar katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Manungu, Turiani mkoani Morogoro.
Mabao ya Azam FC yamefungwa na Ayoub Lyanga yote dakika ya 20 na 54, wakati bao pekee la Mtibwa Sugar limefungwa na Said Ndemla dakika ya 80.
Kwa ushindi huo, Azam FC inafikisha pointi 36 na kupanda nafasi ya nne, ikizidiwa pointi moja na Namungo FC baada ya wote kucheza mechi 25, wakati Mtibwa Sugar inabaki na pointi zake 28 za mechi 25 pia nafasi ya 10.
0 comments:
Post a Comment