KIUNGO wa Ghazl El Mahalla SC ya Misri, Himid Mao Mkami amerejeshwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars kwa ajili ya michezo ya mwanzo ya kufuzu Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwakani.
Akitaja kikosi hicho leo, kocha wa Taifa Stars, Mdenmark Kim Poulsen amewajumuisha pia beki Kennedy Juma na viungo Muzamil Yassin, wote wa Simba, Farid Mussa na Salum Abubakar ‘Sure Boy’ wa Yanga SC.
0 comments:
Post a Comment