• HABARI MPYA

    Sunday, June 14, 2026

    MZALIWA WA KIGOMA AFUNGA BAO KOMBE LA DUNIA AUSTRALIA YASHINDA 2-0

    TIMU ya Australia imeilaza Uturuki mabao 2-0 katika mchezo wa Kundi D Fainali za Kombe la Dunia Asubuhi ya leo Uwanja wa BC Place, Vancouver Jiji liliopo Magharibi mwa Canada.
    Mabao ya Australia yamefungwa na winga wa Watford ya England, Nestory Irankunda dakika ya 27 na kiungo wa FC St. Pauli ya Ujerumani, Connor Isaac Metcalfe dakika ya 75.
    Mfungaji wa la kwanza la Aussie, Nestory Irankunda mwenye umri wa miaka 29 ni mzaliwa wa Kigoma, Tanzania ambako wazazi wake walihamia baada ya kukimbia vita ya wenyewe kwa wenyewe nchini kwao, Burundi.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MZALIWA WA KIGOMA AFUNGA BAO KOMBE LA DUNIA AUSTRALIA YASHINDA 2-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top