KIUNGO Zawadi Peter Mauya amesaini mkataba wa miaka miwili kuendelea kuchezea klabu ya Yanga hadi msimu wa 2024.
Zawadi alijiunga na Yanga mwaka 2020 Julai akitokea Kagera Sugar na baada ya kazi nzuri katika misimu yake miwili ya awali ikiwemo kufunga bao pekee la ushindi katika mechi ya Ligi Kuu dhidi ya watani, Simba Julai 3, mwaka jana amepewa nafasi nyingine Jangwani.
0 comments:
Post a Comment