• HABARI MPYA

    Thursday, May 26, 2022

    YANGA YAWASIMAMISHA NTIBANZOKIZA NA AMBUNDO


    KLABU ya Yanga imewasimamisha wachezaji wake wawili, Dickson Ambundo na Mrundi Saido Ntibanzokiza kuelekea mechi ya Fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) dhidi ya watani, Simba SC Jumamosi Uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza.
    Viungo hao washambuliaji wanadaiwa kutoroka kambini Jumatatu usiku mara baada ya mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Biashara United hapo hapo Kirumba anbayo iliisha kwa sare ya 1-1.
    Na kwa kosa hilo, kocha Mtunisia Nasredin Mohamed Nabi aliamuru warejeshwe Dar es Salaam wakati Yanga inakwenda kambini Shinyanga.
       


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA YAWASIMAMISHA NTIBANZOKIZA NA AMBUNDO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top