• HABARI MPYA

    Thursday, May 05, 2022

    MCHA APIGA MBILI DODOMA JIJI YAITANDIKA BIASHARA 3-1


    WENYEJI, Biashara United wamechapwa mabao 3-1 na Dodoma Jiji FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo Uwanja wa Nyamagana Jijini Mwanza.

    Mabao ya Dodoma Jiji yamefungwa na Khamis Mcha ‘Vialli’, mawili dakika ya 15 kwa penalti na dakika ya 35 na Anuary Jabir dakika y 48, wakati la Biashara United limefungwa na Omary Chinada dakika ya 25.
    Dodoma Jiji inafikisha pointi 27 katika mchezo wa 22 ikisogea nafasi ya nane, wakati Biashara United inabaki na pointi zake 23 za mechi 22 nafasi ya 12.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MCHA APIGA MBILI DODOMA JIJI YAITANDIKA BIASHARA 3-1 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top