• HABARI MPYA

    Friday, May 20, 2022

    COASTAL UNION YAICHAPA DODOMA JIJI 2-1 MKWAKWANI


    WENYEJI, Coastal Union wameibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Dodoma Jiji FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo Uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.
    Mabao ya Coastal yamefungwa na Abdul Suleiman ‘Sopu’ yote mawili dakika ya saba na 15, wakati la Dodoma Jiji limefungwa na Anuary Jabir dakika ya 23.
    Coastal Union wanafikisha pointi 31 na kusogea nafasi ya tisa, huku Dodoma Jiji ikibaki na pointi zake 28 nafasi ya 11 baada ya wote kucheza mechi 25.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: COASTAL UNION YAICHAPA DODOMA JIJI 2-1 MKWAKWANI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top