WENYEJI, Brighton & Hove Albion wameitandika Manchester United mabao 4-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England jana Uwanja wa The Amex .
Mabao ya Brighton yamefungwa na Moises Caicedo dakika ya 15, Marc Cucurella dakika ya 49, Pascal Gross dakika ya 57 na Leandro Trossard dakika ya 60.
Kwa ushindi huo, Brighton wanafikisha pointi 47 katika mechi ya 36 na kusogea nafasi ya tisa, wakati Man United inabaki na pointi zake 58 za mechi 37 nafasi ya sita.
0 comments:
Post a Comment