TIMU ya AS Roma imetwaa taji la UEFA Europa Conference League kufuatia ushindi wa 1-0 dhidi ya Feyenoord ya Uholanzi, bao Nicolo Zaniolo dakika ya 32 usiku wa jana Uwanja wa Arena Kombetare jijini Tirana nchini Albania.
Ushindi huo unamfanya Mreno, Jose Mourinho aweke rekodi ya kipekee kuwa kocha aliyetwaa mataji yote matatu ya Ulaya – Champions League akiwa na Porto 2003–04, Inter Milan 2009–10 na UEFA Europa League akiwa na Man United 2016–17.
0 comments:
Post a Comment