// Disable text selection (not fully reliable) function disableSelection(element) { element.setAttribute('unselectable', 'on'); element.style.userSelect = 'none'; element.style.MozUserSelect = 'none'; element.style.webkitUserSelect = 'none'; } // Apply to the entire document body document.addEventListener('DOMContentLoaded', function() { disableSelection(document.body); }); THIERRY HENRY ATUNGIKA DALUGA MAREKANI, APANIA KURUDI KIVINGINE ARSENAL - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE THIERRY HENRY ATUNGIKA DALUGA MAREKANI, APANIA KURUDI KIVINGINE ARSENAL - BIN ZUBEIRY SPORTS - ONLINE
  • HABARI MPYA

    Monday, December 01, 2014

    THIERRY HENRY ATUNGIKA DALUGA MAREKANI, APANIA KURUDI KIVINGINE ARSENAL

    MSHAMBULIAJI Thierry Henry ametangaza kuondoka klabu ya New York Red Bulls ya Marekani baada ya kuitumikia kwa miaka minne na nusu katika Ligi Kuu ya nchini humo.
    Mwanasoka huyo wa zamani wa kimataifa wa Ufaransa, ametangaza uamuzi wake huo siku tatu baada ya kukiri anapenda kurudi Arsenal, na kubadilisha picha yake ya bango katika ukurasa wake wa Facebook kwa kuweka picha ya Uwanja wa Emirates.
    Mkongwe huyo mwenye umri wa miaka 37 atatumia wiki chache zijazo kuamua mustakabali wake wa baadaye wa maisha, huku kufundisha klabu katika Ligi Kuu ya England ikiwa moja ya mipango.
    Thierry Henry, pictured celebrating scoring in January 2012, admitted he would love to return to Arsenal
    Thierry Henry, pichani akishangilia bao Januari mwaka 2012, amesema angependa kurejea Arsenal

    MATAJI YA THIERRY HENRY NA KLABU ALIZOCHEZEA

    1994-1999: Monaco (Mechi 105, mabao 20)
    1999-1999: Juventus (Mechi 16, mabao 3)
    1999-2007: Arsenal (Mechi 254, mabao 174)
    2007-2010: Barcelona (Mechi 80, mabao 35)
    2010-2014: New York Red Bulls (Mechi 122, mabao 51)
    2012-2012: Arsenal (mkopo) (Mechi 4, bao 1) 
    1997-2010: Ufaransa (Mechi 123, mabao 51)
    Monaco: Ligue 1, Taji la ubingwa 
    Arsenal: Ligi Kuu (2), Kombe la FA (3), Ngao ya Jamii (2)
    Barcelona: La Liga (2), Kombe la Mfalme, Super Cup ya Hispania, Ligi ya Mabingwa, Super Cup ya Ulaya, Klabu Bingwa ya Dunia
    New York Red Bulls: MLS Kanda ya Mashariki (2), Ngao ya Mashabiki 
    Ufaransa: 1998 Kombe la Dunia, Euro 2000, Kombe la Mabara 2003
    Henry changed his cover photo on Facebook to an image of the Emirates following his announcement
    Henry amebadilisha picha yake ya bango Facebook na kuweka ya Uwanja wa Emirates 

    "Nachukua fursa hii kutangaza kwamba kwa bahati mbaya Jumamosi ilikuwa mechi yangu ya mwisho kwa New York Red Bulls," Henry amesema leo.
    Henry aliliambia jarida la L'Equipe la Ufaransa Ijumaa kwamba atabakia kwenye soka baada ya kustaafu kama mchezaji kwa kugeukia ukocha, ushauri au utendaji.
    Mshindi huyo wa Kombe la Dunia mwaka 1998 amekiri kujuta kushindwa kuisaidia Arsenal kushinda taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya na ndiyo maana anataka kwenda kutoa mchango wake katika klabu ipate mafanikio Ulaya.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: THIERRY HENRY ATUNGIKA DALUGA MAREKANI, APANIA KURUDI KIVINGINE ARSENAL Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top