TIMU ya KMC imeibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam.
Mabao ya KMC leo yamefungwa na Awesu Awesu dakika ya 39 na Waziri Junior dakika ya 45 na ushei, wakati bao pekee la JKT Tanzania limefungwa na Edward Songo dakika ya 85.
Kwa ushindi huo, KMC inafikisha pointi nne, wakati JKT Tanzania inabaki na pointi zake tatu baada ya wote kucheza mechi tatu.
0 comments:
Post a Comment