• HABARI MPYA

    Thursday, September 28, 2023

    NI MAN UNITED NA NEWCASTLE 16 BORA CARABAO CUP


    TIMU ya Manchester United itakutana na Newcastle United katika mchezo wa Hatua ya 16 Bora Kombe la Ligi England, maarufu kama Carabao Cup Oktoba 30 Uwanja wa Old Trafford Jijini Manchester.
    Hayo yatakuwa marudio ya mchezo wa Fainali ya Carabao Cup msimu uliopita, Mashetani Wekundu walipoichapa Newcastle 2-0 Uwanja wa Wembley na kubeba taji hilo.
    Mechi zote za 16 Bora Carabao Cup zitachezwa Oktoba 30 na Liverpool watawafuata AFC Bournemouth, Arsenal watawafuata West Ham United, wakati Chelsea watawakaribisha Blackburn Rovers.
    RATIBA HATUA YA 16 BORA CARABAO 
    Manchester United v Newcastle
    Chelsea v Blackburn 
    Bournemouth v Liverpool 
    Everton v Burnley 
    West Ham v Arsenal
    Mansfield Town v Port Valer
    Exeter City v Middlesbrough 
    Ipswich Town v Fulham 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NI MAN UNITED NA NEWCASTLE 16 BORA CARABAO CUP Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top