TIMU ya Kagera Sugar imeibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Geita Gold katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC Tanzania Bara leo Uwanja wa Kaitaba, Bukoba.
Bao pekee la Kagera Sugar limefungwa na Disan Galiwango dakika ya 90 na ushei huo ukiwa ushindi wa kwanza kwao baada ya kufungwa mechi mbili za awali, wakati Geita imepoteza mechi ya kwanza ikitoka kushinda moja na kutoa sare moja awali.
0 comments:
Post a Comment