• HABARI MPYA

    Tuesday, February 23, 2021

    NGORONGORO HEROES YATUPWA NJE FAINALI ZA AFCON U20 BAADA YA KUCHAPWA 3-0 NA MOROCCO MAURITANIA

    TANZANIA imetupwa nje ya Fainali za Kombe la Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 20, AFCON U20 baada ya kuchapwa mabao 3-0 na Morocco katika mchezo wa Kundi C jana Uwanja wa Olimpiki wa Nouakchott nchini Mauritania.
    Mabao ya Morocco yalifungwa na viungo El Mehdi Moubarik dakika ya nne kwa penalti, Mohammed Amine Essahel dakika ya nane na mshambuliaji Ayoub Mouloua dakika ya 13.
    Tanzania inamaliza na pointi moja nyuma ya Ghana iliyomaliza na pointi nne sawa na Gambia waliomaliza nafasi ya pili, wakati Morocco imeongoza kwa pointi zake saba.
    Ghana imefuzu Robo Fainali za AFCON U20 kama mshindi wa tatu bora zaidi ya washindi wa tatu wa makundi A na B.

    RATIBA YA ROBO FAINALI AFCON U20
    Alhamisi Februari 25, 2021
    Saa1:00 usiku
    Cameroon U20 Ghana U20
    Saa 4:00 usiku
    Burkina Faso U20 Uganda U20
    Ijumaa Februari 26, 2021
    Saa 1:00 usiku
    Morocco U20 Tunisia U20
    Saa 4:00 usiku
    Jamhuri ya Afrika ya Kati. U20 Gambia U20
     
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NGORONGORO HEROES YATUPWA NJE FAINALI ZA AFCON U20 BAADA YA KUCHAPWA 3-0 NA MOROCCO MAURITANIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top