MABAO ya beki Mfaransa, Jules Koundé dk25 na Mcroatia, Ivan Rakitic dk85 jana yaliwapa wenyeji, Sevilla ushindi wa 2-0 dhidi ya Barcelona katika mchezo wa kwanza wa Nusu Fainali ya Kombe la Mfalme, Copa del Rey Uwanja wa Ramón Sánchez Pizjuan.
Timu hizo zitarudiana Machi 3 Uwanja wa Camp Nou. Mara ya mwisho zilikutana katika Robo Fainali ya michuano hiyo miaka miwili iliyopita na Sevilla ilishinda mechi ya kwanza 2-0 kabla ya kwenda kupigwa 6-1 PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment