• HABARI MPYA

    Sunday, February 07, 2021

    AZAM FC KUFUTA UTEJA WAKE KWA SIMBA SC LEO? MECHI IPO LIVE AZAM SPORTS 1 HD KUANZIA SAA 10:00 JIONI

    MECHI mbili za viporo za Ligi Kuu ya Tanzania Bara zinachezwa leo, mabingwa watetezi, Simba SC wakimenyana na Azam FC kuanzia Saa 10:00 jioni Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam #AzamSports1HD na Namungo FC wakiwa wenyeji wa Ruvu Shooting kuanzia Saa 10:00 jioni Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi #AzamSports1HD.
    Mara ya mwisho Azam FC kuifunga Simba SC ilikuwa ni Januari 28, mwaka 2017 waliposhinda 1-0, bao pekee la aliyekuwa Nahodha John Raphael Bocco dakika ya 70 akiupitia mpira ambao beki Mzimbabwe, Method Mwanjali alikuwa ‘anauchezea’ kwenye eneo la hatari na kwenda kumchambua kipa Mghana, Daniel Agyei.   
    Siku hiyo vikosi vilikuwa; Simba SC; Daniel Agyei, Janvier Bokungu/Ibrahim Ajib dk59, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Abdi Banda, Method Mwanjali, Jonas Mkude, Said Ndemla, Jamal Mnyate/Shiza Kichuya dk47, Muzamil Yassin, Pastory Athanas na Juma Luizio/Laudit Mavugo dk65.
    Azam FC; Aishi Manula, Erasto Nyoni, Gardiel Michael, Yakubu Mohammed, Aggrey Morris, Stephan Kingue/Mudathir Yahya dk77, Himid Mao, Joseph Mahundi, Frank Domayo, John Bocco/Abdallah Kheri dk83 na Ramadhani Singano ‘Messi’/Yahya Mohammed dk63.
    Kwa ujumla, katika mechi 24 za Ligi Kuu ambazo timu hizo zimekutana hadi sasa, Simba SC wameshinda 11, Azam FC wameshinda sita na nyingine sita wametoka sare.


    REKODI YA SIMBA NA AZAM FC LIGI KUU:
    P W D L Pts
    Azam FC 24 6 6 11 24
    Simba SC 24 11 6 6 39
    MATOKEO YA MECHI ZILIZOPITA AZAM V SIMBA
    Machi 4, 2020:          Azam FC 2-3 Simba SC
    Oktoba 23, 2019:      Simba SC 1-0 Azam FC
    Mei 13, 2019:            Simba SC 0-0 Azam FC
    Februari 22, 2019:    Azam FC 1-3 Simba SC
    Februari 7, 2018:      Simba 1-0 Azam FC
    Septemba  9, 2017:  Azam FC 0-0 Simba SC (Chamazi)
    Januari 28, 2017:      Simba SC 0-1 Azam FC
    Septemba 17, 2016: Azam FC 0-1 Simba SC
    Mei 1, 2016:              Simba SC 0-3 Azam (Dar)  
    Desemba 12, 2015:  Azam FC 2-2 Simba SC   
    Januari 25, 2015:     Azam FC 1-1 Simba SC  
    Mai 3, 2014:             Simba SC 2-1 Azam FC 
    Machi 30, 2014:       Azam FC 2-1 Simba  
    Oktoba 28, 2013:     Simba SC 1-2 Azam FC  
    Aprili 14, 2013:         Azam FC 2-2 Simba SC   
    Oktoba 27, 2012:      Simba SC 3-1 Azam FC   
    Februari 11, 2012:    Simba SC 2-0 Azam FC
    Septemba 11, 2011:  Azam FC 0-0 Simba SC
    Januari 23, 2011:      Simba SC 2-3 Azam FC
    Septemba 11, 2010:  Azam FC 1-2 Simba SC
    Machi 14, 2010:        Azam FC 0-2 Simba SC  
    Oktoba 24, 2009:      Simba SC 1-0 Azam FC  
    Machi 30, 2009:        Azam FC 0-3 Simba SC
    Okt 4, 2008:              Simba FC 0-2 Azam FC
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM FC KUFUTA UTEJA WAKE KWA SIMBA SC LEO? MECHI IPO LIVE AZAM SPORTS 1 HD KUANZIA SAA 10:00 JIONI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top