MABAO ya Karim Benzema dakika ya 12 na Toni Kroos dakika ya 42 jana yaliipa Real Madrid ushindi wa 2-0 dhidi ya Valencia katika mchezo wa La Liga Uwanja wa Alfredo Di Stéfano Jijini Madrid.
Kwa matokeo hayo, Real Madrid inafikisha pointi 49 baada ya kucheza mechi 23 na kurejea nafasi ya pili, sasa ikizidwa pointi sita na vinara, Atletico Madrid ambao hata hivyo wana mechi mbili mkononi PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment