MABAO ya beki Mfaransa, Nordi Mukiele dakika ya 45, kiungo Muaustria Marcel Sabitzer dakika ya 73 na beki Mjerumani, Vilmos Tamas Orban dakika ya 87 jana yameipa RB Leipzig ushindi 3-0 dhidi ya waburuza mkia Bundesliga, Schalke 04 Uwanja wa Veltins-Arena mjini Gelsenkirchen.
Sasa RB Leipzig inafikisha pointi 41 na kuendelea kukamata nafasi ya pili, ikiwa inazidiwa saba na vinara, Bayern Munich baada ya timu zote kucheza mechi 20 PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment