BAO pekee la kiungo Mtaliano, mzaliwa wa Brazil, Jorge Luiz Frello Filho 'Jorginho' kwa penalti dakika ya 24 jana liliipa ushindi wa 1-0 Chelsea dhidi ya wenyeji, Tottenham Hotspur Uwanja wa Tottenham Hotspur Jijini London katika mchezo wa Ligi Kuu ya England.
Ushindi huo wa pili mfululizo chini ya kocha mpya, Thomas Tuchel unaifanya Chelsea ifikishe pointi 36 baada ya kucheza mechi 22 na kusogea nafasi ya suta kwenye msimamo, juu ya Tottenham na Everton PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment