• HABARI MPYA

    Sunday, February 07, 2021

    RONALDO AFUNGA AKISHEREHEKEA MIAKA 36 YA KUZALIWA, JUVE YAUA


    MABINGWA watetezi, Juventus jana wameichapa AS Roma 2-0, mabao ya Cristiano Ronaldo na Roger Ibanez aliyejifunga katika mchezo wa Serie A Uwanja wa Allianz mjini Torino.
    Ronaldo alifunga bao lake la 17 msimu huu akitoka kusherehekea kutimiza miaka 36 ya kuzaliwa na sasa Juve inafikisha pointi 42 baada ya kucheza mechi 20 na kusogea nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Serie A, ikizidiwa pointi tano na vinara, Inter Milan ambao hata hivyo wamecheza mechi moja zaidi mbele ya AC Milan yenye pointi 46 za mechi 20 pia
     
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: RONALDO AFUNGA AKISHEREHEKEA MIAKA 36 YA KUZALIWA, JUVE YAUA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top