• HABARI MPYA

    Friday, February 19, 2021

    SERENA WILLIAMS ALIA BAADA YA KUTOLEWA AUSTRALIAN OPEN

    ENA WS

    MKONGWE Serena Williams jana alimwaga machozi kwenye mkutano na wana habari baada ya kutolewa katika Nusu Fainali ya Australian Open na Naomi Osaka akisema alifanya makosa mengi.
    Lakini Serena akakanusha kwamba hiyo ni michuano yake ya mwisho baada ya kuchapwa seti mbili mfululizo (6-3 6-4) na Osaka aliyezima ndoto na binti Williams kutwaa taji la 24 la rekodi Grand Slam.
    Naomi atakutana na mchezaji bora namba 22 duniani, Jennifer Brady aliyetinga fainali yake ya kwanza ya Grand Slams Australian Open baada ya kumfunga mchezaji namba 25, Karolina Muchova seti 2-1 (6-4, 3-6, 6-4) uwanja wa Rod Laver Arena, Jijini Melbourne, Australia PICHA ZAIDI GONGA HAPA


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SERENA WILLIAMS ALIA BAADA YA KUTOLEWA AUSTRALIAN OPEN Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top