MABAO ya Robert Lewandowski dakika ya 17 na 85 jana yaliwapa mabingwa wa Ulaya, Bayern Munich uahindi wa 2-0 dhidi ya mabingwa wa Afrika, Al Ahly katika Nusu Fainali ya Klabu Bingwa ya Dunia Uwanja wa Ahmed bin Ali Jijini Al Rayyan, Qatar.
Sasa Al Ahly watamenyana na bingwa wa Amerika Kusini, Palmeiras ya Brazil kuwania nafasi ya tatu Saa 12:00 jioni, wakati Bayern Munich itamenyana na bingwa wa Amerika Kaskazini Tigres UANL ya Mexico katika fainali Saa 3:00 usiku, mechi zote zikipigwa Alhamisi Uwanja wa Education City Jijini Al Rayyan PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment