• HABARI MPYA

    Friday, September 10, 2021

    MASHABIKI RUKSA YANGA NA RIVERS UNITED

     HATIMAYE Yanga SC imeruhusiwa kuingiza mashabiki katika mchezo wake dhidi ya Rivers United ya Nigeria.
    Yanga SC watakuwa wenyeji wa Rivers United Jumapili Saa 11:00 jioni katika mechi ya kwanza ya Raundi ya Awali Ligi ya Mabingwa Afrika Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam kabla ya timu hizo kurudiana Septemba 19 Uwanja wa Adokiye Amiesimaka Jijini Port Harcourt, Nigeria.
    Na leo imetaja viingilio vya mechi hiyo ambavyo ni Sh. 30,000 VIP A, 20,000 VIP B, 10,000 VIP C na 5,000 kwa mzunguko.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MASHABIKI RUKSA YANGA NA RIVERS UNITED Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top