• HABARI MPYA

    Monday, September 27, 2021

    ARSENAL YAITANDIKA SPURS 3-1 EMIRATES


    WENYEJI, Arsenal wameibuka na ushindi wa 3-1 dhidi ya Tottenham Hotspur katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Jumapili Uwanja wa Emirates Jijini London.
    Mabao ya The Gunners yamefungwa na Emile Smith Rowe dakika ya 12, Pierre-Emerick Aubameyang dakika ya 27 na Bukayo Saka dakika ya 34, wakati la Spurs lilifungwa na Son Heung-Min dakika ya 79.
    Kwa ushindi huo, timu ya kocha Mikel Arteta inafikisha pointi tisa na kupanda nafasi ya 10 ikilingana kila kitu na Spurs sasa baada ya wote kucheza mechi sita.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSENAL YAITANDIKA SPURS 3-1 EMIRATES Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top